Syria imeishutumu Israel kuwa inawasaidia wapiganaji kijeshi, baada ya Israel kushambulia maeneo kando ya Damascus.
Hili ni shambulio la pili kufanywa nchini Syria katika siku chache.
Israel haikusema kitu.
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya nchi za Kiarabu, Nabil al-Arabi, amelaani kile alichoita uhasama wa wazi wa Israel.
No comments:
Post a Comment