Sunday, June 2, 2013

Maelfu ya waandamanaji wameandamana katika barabara za mjini Addis Ababa, Ethiopia, wakidai waandishi wa habari na wanaharakati walioko kizuizini wafunguliwe.
 
Waziri Mkuu wa Ethiopia, Hailemariam Desalegn katika mkutano wa AU hivi karibuni
                     Waandishi wa habari wanasema ni nadra kuonesha upinzani wa namna hiyo kwa chama tawala ambacho kinadhibiti shughuli za jamii sawasawa.
Makundi ya kutetea haki za kibinaadamu yanasema serikali imetumia sheria za kupambana na ugaidi ili kuwafunga waandishi wa habari.

Waandamanaji- wengi kutoka upinzani - walipiga kelele kudai uhuru na haki.
Haya ni maandamano ya kwanza tangu mwaka wa 2005 ambapo mamia ya waandamanaji waliuliwa katika ghasia zilizofuatia uchaguzi.

No comments:

Post a Comment