Saturday, June 1, 2013

Japan yaahidi msaada zaidi kwa Afrika

Japan imeahidi kutoa dola bilioni 32 za msaada na uwekezaji katika Afrika, ikijaribu kulingana na Uchina ambayo ina uhusiano mkubwa zaidi wa kiuchumi na bara hili.
 
Waziri Mkuu Shinzo Abe akikutana na Rais Alassane Ouattara wa Ivory Coast kabla ya mkutano na viongozi wa Afrika
                     Msaada utalenga miradi ya kujenga miundo mbinu na usafiri ndani ya miji pamoja na uzalishaji wa nishati.

Waziri Mkuu wa Japani, Shinzo Abe, aliwaambia wajumbe katika mkutano wa maendeleo ya Afrika unaofanywa mjini Yokohama, kwamba umuhimu utapewa uwekezaji wa kibinafsi.
Alisema: "Mali asili nyingi ya Afrika inatoa fursa muhimu ya biashara na Japan ambayo haina mali asili.

Lakini Japan haitotafuta na kuchimba mali asili kuzileta Japan tu.
Tutaisaidia Afrika ili mali asili ya Afrika ikuze uchumi wa Afrika.
Na soko la Afrika linalokua haraka pia ni muhimu kwa makampuni ya Japan"

No comments:

Post a Comment