Saturday, June 1, 2013

Al-Qaeda wana silaha za kemikali-Iraq

Wakuu wa Iraq wanasema wamegundua njama ya al-Qaeda kutaka kutumia silaha za kemikali nchini Iraq na kuzisafirisha kwa magendo hadi Ulaya na Marekani.
 
Al-Qaeda piya inashutumiwa kuhusika na miripuko wa mabomu Iraq

Msemaji wa wizara ya ulinzi, Mohammad al-Askari, alisema idara ya usalama ya jeshi imegundua karakana tatu za kutengeneza kemikali hizo, pamoja na kemikali ya kuharibu neva.
Bwana al-Askari aliiambia televisheni ya Iraq kwamba wanaume watano walikamatwa baada ya kuchunguzwa kwa miezi mitatu.
Wote walikiri makosa, alisema.

No comments:

Post a Comment