Wachezaji wa Bayern Munich.
Pique amesema licha ya kuwa Messi ndiye mchezaji bora zaidi duniani kwa sasa, hilo halikuwa tatizo la kushindwa kwao.
Messi kutoka Argentina, ambaye amefunga magoli 54 baada ya kucheza mechi 45 msimu huu, alitarajiwa kucheza katika kipindi cha pili kama mchezaji wa ziada hasa baada ya kufunga bao kwenye mechi ya ligi kuu siku ya Jumamosi dhidi ya Althletics Bilbao.
Kocha wa Barcelona Tito Vilanova, amesema mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, alipata jeraha la paja wakati wa mechi yao siku ya Jumamosi na hivyo ingelikuwa hatari zaidi ikiwa angelicheza mechi hiyo akiwa na maumivu.
No comments:
Post a Comment