Sunday, May 19, 2013

Maandamano yazimwa mjini Tunis

Polisi katika mji mkuu wa Tunisia, Tunis, wametumia moshi wa kutoa machozi dhidi ya waandamanaji waliokuwa wakirusha mawe.
 
Maandamano mjini Tunis

Waandamanaji hao ni wa chama cha Waislamu wa msimamo mkali, Ansar al-Sharia, ambao wakijaribu kufanya mkutano wa hadhara uliopigwa marufuku.

Jumatano chama tawala cha Waislamu wa msimamo wa wastani, Ennahda, kilisema mkutano mkuu wa Ansar al Sharia umepigwa marufuku kwa sababu kundi hilo halikupata kibali.
Lakini Ansar al Sharia iliahidi kusonga mbele na mkutano.

No comments:

Post a Comment