Wednesday, July 3, 2013

Mandla ashindwa katika kesi ya makaburi

Mandla ashindwa katika kesi ya makaburi Imebadilishwa: 3 Julai, 2013 - Saa 13:26 GMT Facebook Twitter Google+ Tuma kwa rafiki yako Chapisha .Mjukuu wa Nelson Mandela, Mandla Mandela ameshindwa katika kesi iliyowasilishwa mahakamani dhidi yake kwa tuhuma za kufukua makaburi ya jamaa za familia yake katika mzozo wa makaburi unaokumba familia ya Mandela. Mgogoro huo unahusu maiti za wanawe Mandela watatu ambao Mandla alihamisha na kuwazika karibu na nyumbani kwake zaidi ya miaka miwili iliyopita. Mahakama kuu iliamua kuwa maiti hao lazima warejeshwe katika makaburi yao Jumatano. Mandela anaendelea kuugua hospitalini na haijulikani ikiwa mawakili wa Mandla watakata rufaa dhidi ya uamuzi wa mahakama. Jamaa za familia ya Mandela waliwasilisha kesi ya uhalifu dhidi ya Mandla kwa kosa la uhalifu. Msemaji wa polisi, Mzukisi Fatyela aliambia BBC kuwa maafisa wa usalama watachunguza tuhuma dhidi ya Mandla za kufukua makaburi kinyume na sheria Inahusisha maiti za watoto watatu wa Mandela ambao inaaminika walifukuliwa na Mandla kutoka makaburi ya familia miaka miwili iliyopita. Familia ya Mandela, inataka kurejesha miili hiyo katika kijiji cha Qunu, ambako Mandela, ambaye anaumwa sana hospitalini anataka kuzikwa akifa. Kesi hiyo iliyosikilizwa katika mahakama kuu ya Mthatha, katika mkoa wa Mashariki iliahirishwa hapo jana lakini hukumu ikitaolewa Jumatano. Wiki jana, mahakama ilitoa amri ya muda kwa maiti za watatu hao kuhamishwa kutoka nyumbani kwa Mandla katika kijiji cha Mvezo hadi Qunu, umbali wa kilomita 22. Lakini Mandla Mandela, ambaye alitawazwa kama kiongozi wa kijamii na babu yake, sasa anapinga vikali amri hiyo.

No comments:

Post a Comment