Sunday, June 23, 2013

Snowden atua Moscow

 

Edward Snowden.

Ndege iliyombeba mtaalamu wa zamani wa shirika la ujasusi la Marekani, Edward Snowden imetua mjini Moscow baada ya kusafiri kutoka Hong Kong.

Chanzo kutoka ndege hiyo ya taifa la Urusi kimesema bwana snowden anayetakiwa na Marekani kwa mashtaka ya wizi wa siri za serikali amepanga kuondoka hapo kesho jumatatu kuelekea nchini Cuba kabla ya kuelekea Venezuela ambako amepanga kuomba hifadhi.

Mamlaka ya Hong Kong imesema bwana Snowden aliondoka kwa hiyari yake mwenyewe na kisheria baada ya kugundua njama za kutaka kumkamata zinazofanywa na mtandao wa kijasusi wa marekani kambi ya Uchina.
Hong Kong imesema imeyakataa maombi ya marekani ya kutaka kumkamata na kumrejesha bwana Snowden nchini Marekani kwa nguvu kwa kuwa maombi hayo hayaendani na sheria za ndani za nchi hiyo.
              
 

No comments:

Post a Comment