Friday, May 24, 2013

Syria yakubali kuhudhuria mkutano wa amani

 

Hali nchini Syria inaendelea kuzorota huku wahusika kwenye mgogoro wakikosa mwafaka.
 
Urusi imesema kuwa Syria imekubali kuhudhuria mkutano wa kimataifa kuhusu hali nchini humo utakaofanyika mwezi ujao mjini Geneva.
Wizara yake ya mambo ya nje ilisema kuwa serikali ya Syria, itahudhuria mkutano huo ili watu wa Syria wenyewe watafute suluhu kwa mzozo unaoendelea nchini humo.
Hatua hii inakuja baada ya juhudi za kutaka pande zote kwenye mgogoro wa Syria kuhusika na mazungumzo ya amani.
Upinzani rasmi nchini Syria, umefanya mazungumzo kwa siku ya pili, Ijumaa ukitaka kutafuta namna watakavyohusika na kongamano hilo.

"tunaweza kusema kuwa tumepokea ujumbe kutoka kwa serikali ya Syria kuwa itahudhuria kongamano hilo kwa niaba ya watu wa Syria kusukuma ajenda ya amani na mapatano kutumia njia za kisiasa,'' alisema msemaji wa wizara ya mambo ya nje wa Urusi Alexander Lukashevich.
Marekani imeandaa kongamano hilo ili kutafuta mwafaka wa kisiasa kwa mgogoro wa Syria

No comments:

Post a Comment