Monday, May 20, 2013

India na China zaafikiana kuhusu Mpaka

 

Waziri mkuu wa china na mwenzake wa India wameahidi kuunga mkono amani na utulivu.
 
Waziri mkuu wa China yupo India kwa ziara yake ya kwanza ya nje inayoonekana kugubikwa na mzozo wa muda mrfeu wa mpaka kati ya nchi hizo mbili za bara Asia. 
Ziara ya waziri mkuu huyo wa China inajiri wiki kadhaa baada ya kuwepo malalamiko kutyoka kwa umma kufuatia India kukishutumu kikosi cha China kuingia ktika maeneo yake.
Mkwamo huo hatimaye ulitatuliwa kwa amani , lakini umezua mtazamo mwingine wa hatari inayotokana na mzozo kati ya nchi hizo mbili zenye idadi kubwa ya watu.
Zaidi ya miaka hamsini iliyopita tangu nchi hizo zilipigana vita vya muda mfupi, bado nchi hizo hazijakubaliana kuhusu mipaka yao, na India inatuhumu China kwa kudhibiti sehemu kubwa ya ardhi yake.

Waziri mkuu wa India alimpkoea mwenziwe wa China kwa tabasamu na waziri mkuu wa China akisisitiza kwamba lengo kuu la ziara yake ni kujenga imani kati ya nchi zao.
Aidha Li Keqiang amesema kuwa India na China lazima ziimarishe juhudi zake kutuliza mzozo wa muda mrefu katia ya nchi hizo mbili huku akiahidi kuunga mkono juhudi za amani na utulivu

No comments:

Post a Comment