Waziri mkuu wa china na mwenzake wa India wameahidi kuunga mkono amani na utulivu.
Waziri mkuu wa China yupo India
kwa ziara yake ya kwanza ya nje inayoonekana kugubikwa na mzozo wa muda
mrfeu wa mpaka kati ya nchi hizo mbili za bara Asia.
Ziara ya waziri mkuu huyo wa China inajiri wiki
kadhaa baada ya kuwepo malalamiko kutyoka kwa umma kufuatia India
kukishutumu kikosi cha China kuingia ktika maeneo yake.
Mkwamo huo hatimaye ulitatuliwa kwa
amani , lakini umezua mtazamo mwingine wa hatari inayotokana na mzozo
kati ya nchi hizo mbili zenye idadi kubwa ya watu.
Zaidi ya miaka hamsini iliyopita tangu nchi hizo
zilipigana vita vya muda mfupi, bado nchi hizo hazijakubaliana kuhusu
mipaka yao, na India inatuhumu China kwa kudhibiti sehemu kubwa ya ardhi
yake.
Waziri mkuu wa India alimpkoea mwenziwe wa China
kwa tabasamu na waziri mkuu wa China akisisitiza kwamba lengo kuu la
ziara yake ni kujenga imani kati ya nchi zao.
Aidha Li Keqiang amesema kuwa India na China
lazima ziimarishe juhudi zake kutuliza mzozo wa muda mrefu katia ya nchi
hizo mbili huku akiahidi kuunga mkono juhudi za amani na utulivu
No comments:
Post a Comment