Rais Mohammed Morsi.
Washirika wake katika chama cha Muslim Brotherhood, wanasema kuwa mahakama imejaa majaji waliokuwa wanamuunga mkono rais wa zamani Hosni Mubarak.
Nao wapinzani wa Morsi wanasema kuwa anajaribu kujaza nafasi hizo na wafuasi wake.
Mgogoro ulikithiri wiki jana wakati bunge lilipoendelea kujadili mswaada unaonuia kupunguza umri ambao majaji wanaweza kustaafu kutoka miaka 70 hadi 60, hali itakayowaathiri majaji 13,000 na viongozi wa mashtaka.
Mswaada huo pia ungezuia mageuzi katika idara ya mahakama kuhusu mamlaka ya Rais aliyojiongezea mwaka jana.
Maandamano dhidi ya mswaada huo yalipangwa kufanyika Jumatatu ingawa kwa sasa yamefutiliwa mbali.
No comments:
Post a Comment