Bosco Ntaganda.
"Tumefahamishwa hii leo (Jumatatu) kuwa Bosco Ntaganda ameingia Rwanda na kujisalimisha katika Ubalozi wa marekani hapa Kigali", amesema Louise Mushikiwabo
Jenerali Ntaganda amekanusha mashitaka yanayomkabili katika mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Jinai ICC kwamba anahusika na uhalifu wa kivita na ule dhidi ya binadamu.
Hata hivyo Marekani haijatoa tamko lolote kuhusu taarifa hizo za kujisalimisha kwa Jeneral huyo muasi katika ubalozini wake.
No comments:
Post a Comment