Rais Xi Jinping.
Akiongea kabla ya kuondoka, Bwana Xi alisema kuwa nchi hizo mbili "zilikuwa na uhusiano muhimu wa kimkakati" na kwamba wanaongea "lugha moja ".
Akiwa Afrika Kusini, atahudhuria mkutano wa tano wa Brics utakaofanyika mnamo 26-27 Machi. Brics inajumuisha nchi za Brazil, Urusi, India, China and Afrika Kusini – nchi tano muhimu zinazozidi kukua kiuchumi.
Uchina ndiyo nchi inayofanya biashara nyingi zaidi na Afrika, kuliko Marekani na Ulaya.
"Uhusiano kati ya Uchina na Afrika ni wa kina," Bwana Xi alisema.
Xi Jinping alithibitishwa kuwa rais wiki iliyopita.
No comments:
Post a Comment